October 30, 2017


Manchester City inaonekana kuwa ndiyo timu inayotishia amani ya timu  nyingine Ligi Kuu England katakana na mwenendo wao.

City chini ya Pep Guardiola inaongoza msimamo lakini inaonyesha kuwa na rekodi nzuri zaidi.

Ndani ya mechi 10, imeshinda 9 na safe moja tu huku ikiwa na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa 29, mambo linaloifanya timu yoyote inayotaka kuivuka lazima iwe kwa pointi.


Pia mwenendo wa kufunga mfululizo au katika njaa ya mabao kunaifanya City kuwa hatari zaidi Ligi Kuu England. Kwani inaonekana unapokutana na Manchester City hauwezi kujua nani atakudhuru.


Sergio Aguero amepachipa mabao saba kama ilivyo kwa Raheem Sterling na Gabriel Jesus na Leroy Sane kila mmoja amepiga mabao name, maana yake kwa washambulizi hao wane tayari ni jumla ya mabao 30.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic