Uongozi wa Yanga umesema kuna propaganda zinazoandaliwa ili kuwavuruga kwa kuelezwa kuwa wachezaji wanaidai klabu wakati si kweli.
Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amesema kila mchezaji amelipwa posho zake.
“Sitaki kuzungumzia suala la mishahara ya mchezaji yoyote. Hilo ni suala lake na klabu na kila mmoja anajua imekuwaje,” alisema.
Mkwasa amesema kuna watu wameanzisha propanga zinazoandaliwa ili kuwavuruga.
Mkwasa amesema wao wanaendelea kupambana kuhakikisha kila kitu kinakwenda kwa mpangilio mzuri.
0 COMMENTS:
Post a Comment