December 11, 2017



Baada ya Simba kuhusishwa na kutaka kumsajili Mrundi, Nahimana Shassir anayeichezea Rayon Sport, dili hilo limekufa rasmi baada ya Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma kusema hawatamsajili.

Djuma ambaye ni raia wa Burundi, alipendekeza kusajiliwa kwa mchezaji huyo, lakini baada ya kumuangalia zaidi, amejiridhisha kwamba hata akija hatakuwa na msaada wowote.

Djuma amesema: “Nilipendekeza asajiliwe lakini mpaka sasa tumesitisha dili hilo kwa sababu ameshuka kiwango, nimemuangalia kwenye michuano ya Chalenji nimeona hajaisaidia chochote timu yake, hivyo hatutamsajili tena.

“Hatuwezi kumsajili mchezaji wakati uwezo wake ni mdogo kuliko wale waliopo ndani ya kikosi chetu cha sasa.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic