Wakala wa kuuza wachezaji aliyekuwa anatambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa, Dk Damas Daniel Ndumbaro ameshinda kugombea ubunge katika jimbo la Songea mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Dk Ndumbaro ambaye aliwahi kuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ameshinda kuwania ubunge baada ya kuingia tatu bora akishika nafasi ya tatu na baadaye akapitishwa na kamati kuuu, leo.
Mwanamichezo huyo pia mwanasheria maarufu nchini na mmoja wa mawakili ambao wamekuwa wakifanya vema mahakamani.
0 COMMENTS:
Post a Comment