January 26, 2018



Watani wa jadi Simba na Yanga, kesho Jumamosi watakuwa kitu kimoja kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaowakutanisha Azam na Yanga kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Watani hao watakuwa kitu kimoja kwani Simba inahitaji kuendelea kukaa kileleni bila ya wasiwasi, huku Yanga ikihitaji kuzisogelea timu zilizokuwa juu yake katika harakati zake za kutetea ubingwa wa ligi hiyo.

Kwenye msimamo wa ligi hiyo, Simba inaongoza ikiwa na pointi 32, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 30, huku Yanga ikiwa na pointi 25 katika nafasi ya tatu.

Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten, amesema: “Tumesikia Simba kesho watakuja kutushangilia, niseme tu hii si mara ya kwanza wao kutushangilia, wameshatushangilia mara nyingi, ni jambo jema, sisi ni watani wa jadi na hakuna uadui kati yetu.


“Tunawakaribisha kwani mpira wa miguu ni mchezo wa kiungwana, hakuna jambo baya, tunawashukuru kwa kujitolea kwao.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic