March 12, 2018


Baada ya kuitandika Stand United, kikosi cha Yanga kitaondoka usiku wa leo kuelekea Gaborone, Botswana, kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers FC.

Yanga itaondoka na msafara wa wachezaji 20 pamoja na viongozi 11 kuelekea Botswana ambapo mchezo huo utapigwa Machi 17 2018.

Katika mechi ya awali iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Yanga ilikubali kichapo cha mabao 2-1, hivyo sasa watalazimika kushinda zaidi ya mabao mawili, iwe 2-0, 3-0 au 4-1 ndiyo wataweza kusonga mbele.

Saleh Jembe Blog inawatakia kila la kheri Yanga kuelekea mchezo huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic