March 6, 2018


Na George Mganga

Manchester United imerudi kwenye nafasi yake ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Crystal Palace.

Mchezo huo ambao ulikuwa na matokeo hasi kwa Manchester United katika kipindi cha kwanza, ulimalizika huku Palace akiwa na bao moja lililofungwa na Townsend dakika ya 11.

Mpaka mapumziko Palace alikuwa mbele kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili kilipoanz, Palace walifunga bao la pili na kuufanya mchezo uwe mgumu kwa United baada ya van Aanholt kufunga bao dakika ya 48 ya mchezo.

United walirudi kwa kasi mnamo dakika ya 55 Smalling alifunga, baadaye dakika ya 76 Lukaku naye akacheka na nyavu na mchezo kuwa sare ya 2-2.

Dakika za mwisho kabisa ikiwa imeongezwa moja mchezo umalizike, Matic alipigilia msumari wa mwisho na kufanya matokeo yawe 2-3.

United sasa imerudi tena nafasi ya pili kwa kufikisha alama 62, juu ya Liverpool iliyo na 60.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic