May 18, 2018


Na George Mganga

Uongozi wa klabu ya Yanga kupitia kwa Katibu wake, Charles Boniface Mkwasa, umesema yauari umeshamalizana na wachezaji watatu watakaokuwa na timu hiyo.

Mkwasa ameeleza kuwa watawataja wachezaji hao siku za hivi karibuni ambao watakuwa mhimili mkubwa katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga ilipewa nafasi tatu na CAF kusajili wachezaji ili kukipa nguvu kikosi chao ambapo kipo kwenye mashindano hayo ya kimataifa.

Mkwasa amesema hataweza kuwaweka wazi wachezaji akidai wanaweza wakapokonywa na baadhi ya klabu za hapa nchini hivyo wakati ukifika utawataja.

Juzi Jumatano Yanga imekwenda sare na Rayon Sports ya Rwanda ikiwa ni mchezo wa pili wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Wakati huo timu hiyo ipo njiani hivi sasa kuelekea Shinyanga kwa ajili ya mechi ya ligi dhidi ya Mwadui FC itakayopigwa Uwanja wa CCM Kambarage.

Kutoka Spoti Leo - Radio One.

6 COMMENTS:

  1. Ushauri wanu ulikuwa kwa Pappy Kambale, Lubinda Mumbia na Kotinyo....Au Mohamed Rashid na Mpepo kutoka Prison...hii nilitoa kutokana na mazoeano na aina ya mpira wa mfanano wa timu zetu kwenye eneo la ushambuliaji. nataka nione wapi Yanga wamewatoa hao watatu..nikikosa kwenye hilo nitajua

    ReplyDelete
  2. Si hapa, leo yanga imefika hadi kuwa na woga wa kuwataja wachezaji wanaotaka kuwasajili kwa hoja wanaogopa Ukowapi ubabe wa yanga wa kuwanyanyasa simba kwa kuwachukuwa nyota wao kila wanapoamuwa kuwachukuwa. Ubata wa yanga ni kuwa waliondokea kumfanya Manji kama mama kwa mtoto wake mchanga ambaye ndie muhili wa timu na ulipotenguka ni ikawa basi tena.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mbona hata samba inamtegemea mtu mmoja tu.

      Delete
  3. Kutokana maneno ya mkwasa ndio mana lipuli walikuwa na wasiwasi na mchezajiwao kumbe hawana nia ya kuazimwaila walitaka kymsajiri kupitia fimbo njia ya mkato

    ReplyDelete
  4. Duuuuuh!!!!!! Kumbe Lipuli walikuwa sahihi kwa ajili ya kugomea kumtoa mchezaji wao. Sasa Mkwasa unafikia hatua unakataa kutambulisha wachezaji wa aina gani? Sasa ushauri mtaupata wapi jamani?

    Protas-Iringa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic