July 1, 2018




Baada ya kikosi cha Simba kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Dakadaha FC ya Somalia katika mchezo wa Kombe la Kagame jana Jumamosi, wachezaji wapya Simba wageuka gumzo.


Katika mchezo huo ambao Simba walikuwa na wachezaji takribani wote wa kikosi cha pili, uliwang'arisha vijana ambao waliongozwa na mkongwe wao Mwinyi Kazimoto Uwanjani.

Katika safu ya ushambuliaji, Simba ilikuwa na Adam Salamba, Juma Rashidi na Moses Kitandu wakati huo Marcel Kaheza naye akitumika kuwalisha mipira washambuliaji wa mwisho akicheza kama kiungo mshambuliaji.

Adam Salamba, aliweza kuifungia Simba mabao mawili na kuweza kuandika rekodi yake kuifungia klabu hiyo kongwe katika mchezo wake wa kwanza kwenye Uwanja wa Uhuru.

Uwepo wa wachezaji hao unaleta taswira mpya ya kikosi cha Simba ambacho kinaweza kuwa tishio baadaye endapo vijana hao wataendelea na kasi waliyoanza nayo.

Kikosi hicho pia kilipewa nafasi katika mashindano ya SportPesa huko Kenya japo hakikuweza kufanya vizuri kutokana na kutokuwa kambini kwa mrefu suala lililosababisha kukosa muunganiko mzuri.

Yawezekana ikawa ni mapema zaidi kukipa kipimo dhidi ya Dakadaha walioonekana kuwa dhaifu, tujaribu kukiangalia kwenye michezo mingine kwa kuwa bado mashindano yanaendelea.


1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic