July 2, 2018


Wolves wamejaribu kumasaini kiungo wa kati wa Colombia Juan Quintero ambaye ameonyesha mchezo mzuri kwenye Kombe la Dunia nchini Urusi lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Real Madrid na Tottenham kwa mchezaji huyo wa miaka 25. (Mirror)

Chelsea wanamteua meneja mpya Maurizio Sari leo Jumatatu na mchezaji ambaye atamsaini kwanza ni kiungo wa kati wa Urusi Aleksandr Golovin, 22, ambaye atagharimu pauni milioni 27 kutoka CSKA Moscow. (Sun)

West Ham na Fulham wanamenyana kwa pauni milioni 25 kumsaini mshambuliaji wa Nice Mfaransa Alassane Plea, 25. (Sun)

Newcasle pia nao wanammezea mate mshambuliaji wa zamani wa Lyon Plea, ambaye alifunga mabao 21 kwenye mashindano ya msimu uliopita. (Shields Gazette)

Newcasle wanatathmini ofa kwa wing'a wa Crystal Palace muingereza Andros Townsend, 26, lakini ikiwa tu wataamua kumuuza wing'a msikochi Matt Ritchie, 28, kwenda Stoke City. (Telegraph)

Juventus wamekataa ofa ya Lazio ya pauni milioni 89 na kiungo wa kati wa Uruguay Rodrigo Bentancur, 21 kwa kiungo wa kati wa Serbia Sergej Milinkovic-Savic, 23. (Tuttosport - in Italian)

Matej Vydra anakaribia kuhamia Leeds kwa pauni milioni 11 baada ya mshambuliaji huyo wa miaka 26 kutolewa kutoka kambi wa mazoezi ya Derby huko Tenerife. (Telegraph)
Stuttgart hawatamuuza mlinzi mfaransa Benjamin Pavard, 22, kwa milioni euro 50 na wanataka kumweka mchezaji huyo kwa mwaka mwingine kulingana na mkurugenzi wa klabu hiyo ya Ujerumani. (Stuttgarter Nachrichten - in German)
Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic