July 3, 2018


Wachezaji wa timu ya taifa ya rugby ya Zimbabwe wamelazimika kulala mitaani nchini  Tunisia wakisubiri mechi yao mwishoni mwa wiki hii.

Hali hiyo imesababishwa na hali mbaya ya kifedha na kuifanya timu hiyo iliyo chini ya kocha Peter de Villiers, kulala mitaani.

Zimbabwe  ilifungwa  45-36 na Kenya katika michuano ya awali ya kuwania kushiriki Kombe la Dunia la Rugby iliyofanyika wiki iliyopita  nchini humo.

Habari zinasema timu hiyo ilizuiwa uwanja wa ndege kwa kushindwa kulipia ‘visa’ za kuingia nchini humo ambapo wachezaji walikuwa  hawakulipwa chochote walipokuwa nchini Kenya.

Kuhusu chakula, inasemekana kocha De Villiers ndiye aliwanunulia kwa fedha yake binafsi.

Imeandaliwa na Global Publishers

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic