August 9, 2018


Na George Mganga

Kikosi cha Yanga kimeanza kuonesha ubabe wa mechi zake za kirafiki huko Morogoro kwa kuikandamiza kipigo cha mbwa koko Tanzania Academy cha mabao 5-1.

Katika mchezo huo uliokuwa wa kwanza kwa, mabao ya Yanga yalifungwa na Deus Kaseke, Emmanuel Martin, Maka Edward, Heritier Makambo na Mrisho Ngassa.

Yanga imecheza mchezo huo na kituo hicho cha kukuza vijana ambao ulikuwa ni pendekezo la Kocha Mkongomani, Mwinyi Zahera, kwa ajili ya kuwapima wachezajiw ake vizuri.

Zahera alihitaji timu ya daraja la chini ili kuona wachezaji wake namna walivyopokea mafunzo yake kwa takribani siku tano ambazo wamefikisha Morogoro tangu waweke kambi mjini humo.

Yanga imekipiga na Tanzanite Academy ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Agosti 19.

8 COMMENTS:

  1. Huu utani mwengine haufai Yanga ajibu mapigo kwa Simba kwa kumfunga nani?

    ReplyDelete
  2. Haha haha haha kwa kuwafunga kijana wanaojifunza soka katika kituo cha kuinua soka la vijana wa mjini morogoro (Tanzania Academy) wengi wao wana miaka kati 16 na 17 waliookotezwa katika vitongoji vya Moro

    ReplyDelete
  3. Duuh wakimataifa wanajipima na academy?

    ReplyDelete
  4. Duuh wakimataifa wanajipima na academy?

    ReplyDelete
  5. Yanga yapeleka salamu kwa Simba kwakuishibisha magoli timu kali ya mchangani. Tutakumbuka kuwa Kocha Zahera alitamka kuwa watafanya sapraizi na kweli wameifanya na hiyo ni pia kwa wale walioukwa wakijiona nyota na walo waliotakia mabaya yanga kudhani bila yao yanga itashindwa. Wakae upande wawaache wanaume kaxi yao

    ReplyDelete
  6. Ukiwa na wachezaji wapya na msimu mpya ndio inavyotakiwa unaanz na team dhaifu.
    Mfano Everton ameifunga timu ya mchangani goli 22 pia Arsenal alishinda goli 8-0 alikazarika Simba dhidi ya timu ya umoja wa madereva wa waendesha Tax wa Kiparestina nchini Uturuki

    ReplyDelete
  7. Huyu mwandishi boya kweli kweli

    ReplyDelete
  8. Hivi nyie wanasimba mnapenda kushadadia mambo ya yanga hivi nyinyi mbona mlecheza na umoja wa madereva tax wa kipalestana uturuki alafu yanga wako kimya na wiki end hii mnaenda kucheza na timu kutoka ruandwa ligi sijui hiyo barcelona

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic