September 19, 2018


Baada ya kamati ya Tuzo ya Ligi Kuu Bara kumtaja mshambuliaji wa Simba, Med­die Kagere ameweka wazi kuwa kupata tuzo ya Mche­zaji Bora wa mwezi Agosti ni faraja kwake kutokana na watu kuiona kazi yake.

Kagere alipata tuzo hiyo baada ya kuwazidi wachezaji aliokuwa anashindanishwa nao ambao ni Omary Mponda wa Kagera Sugar mwenye mabao 2 na Joseph Ma­hundi wa Azam FC mwenye mabao 2, huku Kagere akiwa na mabao 3 baada ya kucheza mechi mbili.

Kagere alisema kuwa ni jambo la faraja hasa kwa kazi yake kuweza kuonekana na watu kuithamini hivyo anaamini huo kwake ni mwanzo mzuri na hakuwa na muda wa kumfuatilia Makambo wakati Yanga ilipocheza na Stand United.

“Nina­washukuru sana ambao wameniteua na kunipa tuzo hiyo ya mchezaji wa mwezi nase­ma Asante, ila mafanikio haya ni kwa ajili ya timu yangu na mashabiki ambao wapo pamoja nasi bega kwa bega.

“Kila baada ya kumaliza mchezo mmoja natambua kuwa kuna mwingine un­akuja hivyo napenda sana kuwashukuru, kuhusu kutumia muda wangu kutaza­ma mchezo wa Yanga sijafan­ya hivyo kwa kuwa nilikuwa nafuatilia ligi ya Ulaya” al­isema Kagere aliyekipiga Gor Mahia ya Kenya kabla ya ku­tua Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic