October 21, 2018


Timu ya Simba imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Stand United mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa leo ikiwa ni kulipa kisasi kwa wapinzani wao Yanga ambao nao walishinda kwa idadi ya mabao hayo jana.

Kiungo mchezeshaji  Clatous Chama, mshambuliaji wa kimataifa Emanuel Okwi na kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya wamewanyanyua mashabiki wa  Simba .

Chama amefunga bao lake la kwanza dakika ya 31,amemtengenezea pasi ya bao Okwi dakika ya 45,Kichuya  baada ya kupiga kona dk ya 77,mchezaji wa Stand United Eric Mulillo alijifunga na kuhitimisha ushindi mnono kwa Simba.


4 COMMENTS:

  1. Kwa kweli ligi ni ngumu na kila inapopatikana nafasi Simba inabidi kushinda, ikumbukwe imeshaharibu mechi moja ya kule Mwanza. Kila la heri Simba kwenye mchezo wa leo.

    Protas-Iringa

    ReplyDelete
  2. Hayo ndiyo maajabu sasa na stendi hawakufunga hata goli moja...timu iliyo namba 7 kuifunga iliyo namba 11.Siyo iliyo namba 3 ikiwafunga vibonde vya ligi mnatuandikia eti wamefanya maajabu...Saleh mnaboa timu yenu ikishinda vichwa vya habari mnavirembesha mnavipamba mpaka vinaboa.Timu zingine zikishinda ni habari ya kawaida.blog yenu inatia aibu

    ReplyDelete
  3. Huo ndio umbumbu wa uandishi,like no own gaol LA erick murilo,unatuambiaje kichuya kafunga.Naona hukuwepo uwanjan hata azm hujaangalia tens unasfia,kona ya moja kwa moja,kuwa making kaka na uandishi wako,acha muisifie vyura fc but simba tupo juu zaid yao

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic