October 13, 2018


Jose Mourinho anataka Manchester United ifufue uhamisho wa Sergej Milinkovic-Savic Lazio baada ya ofa ya Euro milioni 80 dhidi ya kiungo huo wa kati wa Serbia kugonga mwamba msimu wa joto. (Sun)

Newcastle inatafakari uhamisho wa meneja wa Celtic Brendan Rodgers kuchukua nafasi ya Rafael Benitez katika uga wa at St James Park. (Mirror)

Manchester United imewasiliana na meneja wa Juventus Massimiliano Allegri huku tetesi kuhusu hatima ya Jose Mourinho uwanjani Old Trafford zikiendelea . (Calciomercato, via Express)

West Ham inawazia uhamisho wa mwezi Januari wa mlinzi wa Chelsea na England Gary Cahill,32, ambaye kandarasi yake inakamilika msimu wa joto. (Mirror)


Manchester United imetangaza ofa ya kumnunua beki wa kushoto wa Napoli na Algeria Faouzi Ghoulam, 27. (Calciomercato, via Manchester Evening News)

Mourinho pia anapania kumrudisha Manchester United, mshambulizi wa zamani wa Uswidi ambaye sasa anachezea LA Galaxy Zlatan Ibrahimovic, 37, mweiz Januari mwakani. (ESPN)

Kambi ya David de Gea , 27, ina matumaini kuwa kipa huyo wa Uhispania atatia saini kandarasi mpya na klabu ya Manchester United. (Manchester Evening News)


Atletico Madrid inammezea mate kiungo wa kati wa Chelsea na timu ya taifa ya Uhispania Cesc Fabregas, 31. (Mirror)

Eric Bailly yuko tayari kufanya maamuzi yake ya siku zijazo wakati wa majira ya joto ikiwa ndoto yake kujiunga na Manchester United hayaitatimia.


Mlinzi huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 24 ameaza michezo ya ligi tatu msimu huu. (ESPN)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic