October 8, 2018


Kiungo mshambuliaji anayeongoza kwa asisti nyingi Yanga, Ibrahim Ajibu, ameibuka na kuwaambia maneno ma­zuri ya kuwatia matumaini mashabiki wa timu hiyo, kwa kutamka kuwa mashabiki wasihofu, mambo mazuri yanakuja.

Kauli hiyo aliitoa ikiwa ni saa chache kabla ya pambano lao dhidi ya Mbao FC ka­tika mchezo wa Ligi Kuu Bara jana Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Cham­pioni Jumatatu, Ajibu alisema wao kama wache­zaji wanatambua umuhimu wa mashabiki wao, hivyo ni lazima wapate matokeo mazuri katika michezo ijayo ya ligi ili kuhakikisha wana­fanikisha malengo yao.

Ajibu alisema, wanafa­hamu ugumu wa ligi uliopo katika msimu huu, lakini watahakikisha wanafanya kila liwezekanalo ku­fanikisha ushindi huku akiwataka mashabiki kuto­kata tamaa kuji­tokeza uwanjani, pale wanapopata matokeo mabaya.

“Tunataka kuona timu yetu ikiendelea kupata matokeo mazuri,” alisema Ajibu.

1 COMMENTS:

  1. Kwa mechi za nyumbani mnajisifu,ngojeni muone ugenini kama mtakohoa,mpira ndivyo ulivyo,labda muendelee kubebwa kama kawaida yenu hii tff imeoza,okwi amekatwa kwenye box tena karibu na goli lakini refa kapeta,coast nao wamefanyiwa hivyo hivyo mechi na azam ila chamsingi ni kuzoea tu kwamba Tanzania mwenye mpira ni yanga pekee labda na hao azam,wasimamiz wa ligi kama hawaoni yanayofanyika.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic