October 12, 2018


Staa wa Juven­tus, Cristiano Ron­aldo amedai kuwa kuna watu walifoji taar­ifa zake kuhusu skendo ya ubakaji inayomuan­dama kwa sasa.

Ronaldo ameweka wazi hayo kupitia mwanasheria wake, Peter Christiansen ambaye amedai kuwa kuna nyaraka ziliibiwa na kutu­mika vibaya kwenye skendo hiyo ili kuonyesha ni kweli mteja wake alibaka kitu am­bacho siyo kweli.

Mwanasheria huyo amesema baada ya nyara­ka kadhaa kuibiwa ziliten­genezwa na kubadilishwa ili ionekane Ronaldo alihusika katika kumshawishi mwa­namke aliyefungua kesi kuwa alilipwa ili akae kimya miaka kadhaa ya nyuma.

Ronaldo, 33, amekuwa akikana mara kadhaa kuhusika katika kumbaka Kathryn Mayorga wakati walipokutana kwenye uku­mbi wa starehe maeneo ya Las Vegas nchini Marekani mwaka 2009 lakini skendo hiyo imeendelea kumuan­dama na kutishia biashara zake binafsi.

Nyota huyo anadai lengo la skendo hiyo ni kumhar­ibia  sifa na jina lake na hakuna ukwe­li wowote.


I l i d a i w a kuwa mwa­ka 2010, R o n a l d o a l i m p a mw amk e huyo pauni 287,000 ili akae kimya kuhusu skendo hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic