October 13, 2018


Dakika 90 za mchezo wa kirafiki baina ya Yanga na Malindi FC umemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mbao 2-0.

Mabao pekee ya mchezo huo yamefungwa na Mrisho Ngassa pamoja na Emmanuel Martin.

Yanga imecheza mechi hiyo visiwani Zanzibar ikiwa ni sehemu ya kumuaga beki wake wa zamani, Nadri Haroub 'Cannavaro' ambaye amestaafu kucheza soka.

Cannavaro ambaye kwa sasa ni Meneja wa timu, ameagwa vema kutokana na timu yake kucheza soka zuri dhidi ya wapinzani kwa kutawala sehemu kubwa ya mchezo huo.

Mbali na kumuaga Cannavaro, Yanga imeutumia pia mchezo huo kama sehemu ya maandalizi kuelekea mechi na Alliance Schools katika Ligi Kuu Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic