January 20, 2019


Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara, ameamua kujifariji kimtindo kwa kukihusisha kipigo walichokipata dhidi ya AS Vita kwa kuwataja Yanga kuwa waliwahi kuwafunga pia.

Simba ilipoteza mchezo huo jana kwa kuchapwa mabao 5-0 ukiwa ni mchezo wa kundi D katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kufuatia kichapo hicho, Manara ameandika kupitia Instagram yake kuwa hata Yanga waliwahi kuwafunga, akisema Simba si ya kwanza kupokea kichapo hicho.

Amewasema Yanga kuwa wasijisahau kwani waliwahi kuwafunga kipindi cha nyuma katika Ligi Kuu Tanzania Bara.


13 COMMENTS:

  1. Yanga siku zote ni ya kupigwa na simba goli 5. Yanga ni mbovu

    ReplyDelete
  2. Tuliomba timu ifanye usajili makini, wao wakasema watamfunga hata Juve akija Taifa.

    ReplyDelete
  3. Daaaaah sisemi sana ila timu yetu bado sana kimataifa Asante Bro Haji tunatambua uwepo wako

    ReplyDelete
  4. Daaaaah sisemi sana ila timu yetu bado sana kimataifa Asante Bro Haji tunatambua uwepo wako

    ReplyDelete
  5. Hongera sana Haji kwa kumbukumbu lakin kwa kilichotokea jana mmmh mtu mwenye hekima angekosa la kusema...!! Unajua zilikuwa zifikie 8?!

    ReplyDelete
  6. Swali kwako Manara,Yanga haijawahi kuifunga Simba 5-0 ligi kuu?

    ReplyDelete
  7. Yanga ndio ilikuwa ya kwanza kuifunga Simba 5-0 katika ligi kuu kabla Simba kulipa kisasi,so huna point hapo ya kutusahaulisha 5G ya jana.

    ReplyDelete
  8. Hapa nilipo wafariji wakubwa ni Stand United tu, nadhani kama nao jana wangepigwa, nina imani leo nisingeamka. Simba yetu ya jana Beki yote mbovu! Hawajui kukaba, wanampa mtu uhuru wa kudrive mpira anavyotaka, wao wanabaki kufukuzia tu kwa nyuma, matokeo yake ndo yale ya Wawa yakasababisha penati. Ukiangalia hata one to one haikuwepo, unakuta wachezaji wa Vita wapo wanne beki zipo 2 au 3. Mda mwingine uvivu wa kukaba mtu mmoja anawapita wachezaji wanne wa simba!. Kocha fundisha kwanza wachezaji namna ya kukaba. Hukuona wenzetu jana wanakaba wawiliwawili? Kingine kocha unatakiwa uwe na mbinu mbadala. Pale kipindi cha kwanza ulipoona mbinu yako imefeli, ulitakiwa kuja na mbinu nyingine kipindi cha pili. Matokeo yake ukaja vilevile, zaidi ukabadilisha wachezaji tu lakini mfumo ukabaki ule ule. Timu ni nzuri ila matatizo makubwa kwao ni hawajui kukaba kwa jihadi, pasi hazifiki, kuna wakati wanapoozesha mchezo, na pia tatizo kwako kocha ni mfumo ulionao ni mmoja tu, jiongeze. Ukisikia Timu 16 bora barani Afrika sio mchezo, maana yake unakutana na timu makini na zinazotumia kosa lako moja tu kukuumiza. Sio sawa na mechi zenu za ligi huku unacheza na azam au yanga au ndanda, timu inafanya makosa 10 na mpinzani hatumii hata kosa moja kupata goli!.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Maneno yako ni swadkta.Bado nashangaa kwa nini benchi la ufundi halina kocha msaidizi toka aondolewe Djuma?Kocha mmoja ni ngumu kuwamudu wachezaji waliosajiliwa zaidi ya 24.
      Kuna wachezaji wetu hapo Simba hawajafikia kiwango cha kupambana ktk ligi hii ya mabingwa ya Africa.Tunahitaji usajili madhubuti kweli-kweli na sio mzaha na wachezaji wanaojitoa hasa kwa kucheza jihadi.Majority ya wachezaji wetu hawana nguvu na hili naliona hata kwenye ligi yetu.Ukweli timu ya AS VITA imekamilika na wachezaji wanapambana hasa kudhihirisha kuwa wao ni proffesional team na nimewafuatilia michezo yao takribani sita walizocheza nazo ...dah kwa kweli wako vizuri sio masihara.Klabu zetu za bongo tatizo ni wachezaji wenyewe kutojituma na sio makocha.Nawavulia kofia AS VITA kwani hawabatishi.

      Delete
  9. Toa sababu za msingi wewe kijana muongeaji saaana. Umeona ilivyo aibu kuongea ongea bila kuwa na utaalamu? Mambo ya Yanga hayausiani na kipigo hicho

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic