January 22, 2019





Mlinda mlango namba moja wa Yanga, Klaus Kindoki amekubali kuokota mipira mara tatu nyuma ya nyavu katika mchezo wa michuano ya SportPesa Cup ambao umechezwa Uwanja wa Taifa

Yanga imecheza na KK Sharks ya Kenya na tayari Kindoki amegeuka mara tatu baada ya kuanza mapema dakika ya 12 kupitia kwa Abuye Duke na  kugeuka tena dakika ya 36 kupitia kwa Abege George.

KK Sharks walirejea kipindi cha pili wakiwa wanaongoza kwa mabao 2-0 ambayo waliyapata katika kipindi cha kwanza baada ya kushambulia.

Kipindi cha pili dakika ya 87 Yanga walifunga bao la kufutia machozi kupitia kwa Amiss Tambwe hali iliyoamsha ari kwa KK Shark kufunga bao la tatu dakika ya 90 kupitia kwa Abuye Duke.

Lakini Yanga waliamka na kufunga bao la pili ndani ya dakika za lala salama kupitia kwa Herieter Makambo.

Kesho ni zamu ya Simba kumenyana na AFC Leopards Uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 na Mbao watafungua dimba saa 8:00 mchana kwa kumenyana na mabingwa watetezi Gor Mahia.

5 COMMENTS:

  1. Eti Zahera atachukua makombe yote! Hata FA cup asahau..nadhani baada ya kipigo cha Stand united na hiki atajua mpira hauchezwi kwa maneno. Kuna makocha hapa Tanzania hawaongei ongei

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama kocha Babu Hans Plujim haongei

      Delete
  2. Walisusa kupeleka kikosi cha kwanza kujiandaa na Ligi kuu pamoja na Sportpesa,lakini waaapi,vipigo vinawaandama. Hahahahahahaaa

    ReplyDelete
  3. Na mambo bado....wakichomoa hizo mechi tano za ugenini...hongera yao

    ReplyDelete
  4. Kwa hiyo saleh jembe hayo ndiyo matokea mnatupatia kwa kichwa cha habari hicho? Si na Singida United mgeaandika hivyo hivyo? Au kwa kuwa timu yenu imefungwa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic