February 7, 2019


Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania, Boniface Wambura, amesema kuwa ligi ilipofikia imebanana kiasi cha baadhi ya timu kutofautiana idadi ya mechi walizocheza.

Wambura ameeleza kuwa kumekuwa na mashindano mengi hivi karibuni ambayo yamesababisha ratiba hiyo kupangwa na kupanguliwa hivyo mechi kushindwa kwenda kama ilivyokuwa imepangwa awali.

Kauli ya Wambura imekuja mara baada ya Kocha Mkuu wa Yanga kuutumia lawama uongozi wa TFF kuwa wanaionea Yanga kwa namna ambavyo ratiba hiyo inakwenda hivi sasa.

Kiongozi huyo amesema hakuna namna kwa vile kulikuwa na muingiliano wa mashindano ikiwemo Simba ambayo inashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika kucheza mechi chache mpaka sasa.

"Ni kweli ratiba imebanana zaidi hivi sasa ukiangalia kulikuwa na mashindano mengi ambayo yalileteleza kupangwa na kupanguliwa kwa ratiba, tunapambana kwa namna tuwezavyo ili kila kitu kikae vizuri" alisema Wambura.

4 COMMENTS:

  1. TFF acheni kuwasikiliza sana hawa Yanga, tayari maji yamewafika shingoni kutokana na kuanza kutoka nje ya Dar na kupata matokeo ambayo hawakuyatarajia kuyapata. Hayo ni malalamiko tu yasiyo na tija, mnadhani kama Yanga wangeshinda Tanga na jana Singida wangetoa malalamiko kama haya? Wao wanajiona kama ni Miungu ya ushindi tu. Lazima wakubaliane na matokeo bhana, ratiba ni ngumu kwa timu zote, sio Yanga pekee, kwanini walalamike wao tu! au kwavile mbao hawana wa kumlalamikia, au kwa vile Biashara hana wa kumlalamikia! Mzunguko wa kwanza timu kama Biashara karibu zaidi ya nusu ya mechi 19 walicheza nje ya Musoma, na walipoteza mechi karibu zote na kutoa sare kutokana na kucheza nje ya kwao, hawakulalamika, iweje hawa Yanga walalamike sana! Au wanataka TFF wafanye kama wanavyotaka wao!!?. Na bado. Yaani hapa mechi 5 mnachukua pointi 3 tu!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nyinyi mlikalili upande mmoja wa shilingi, tumehamia upande wa pili wa shilingi sasa, kubalianeni na kila takwa la upande huu wa pili wa shilingi. Kulalamika sana hakuwezi kuwaponya, zaidi niwashauri tu anzeni kuimba mapambio ya niagieni.

      Delete
  2. Hizi hapa ratiba za Simba na Yanga kwa mwezi huu Februari 2019

    SIMBA SC

    ��07/02/2019
    Simba vs Mwadui - Dar

    ��12/02/2019
    Simba vs Al Ahly - Dar

    ��16/02/2019
    Yanga vs Simba - Dar

    ��19/02/2019
    Africa Lyon vs Simba - Arusha

    ��22/02/2019
    Azam vs Simba - Dar

    ��26/02/2019
    Lipuli vs Simba - Iringa

    ��03/03/2019
    Stand United vs Simba - Shinyanga

    ��09/03/2019
    Js Saoura vs Simba - Algeria

    ��16/03/2019
    Simba vs As Vita - Dar

    ��18/03/2019
    Simba vs Ruvu Shooting - Dar

    ��31/03/2019
    Simba vs Mbao - Dar

    YANGA SC

    ��06/02/2019
    Singida United vs Yanga -Singida

    ��10/02/2019
    JKT Tanzania vs Yanga -Tanga

    ��16/02/2019
    Yanga SC vs Simba -Dar

    ��20/02/2019
    Mbao vs Yanga -Mwanza

    ��25/02/2019
    Namungo vs Yanga -Lindi

    ��02/03/2019
    Alliance School vs Yanga Mwanza

    ��10/03/2019
    Yanga vs KMC -Dar

    ��16/03/2019
    Lipuli FC vs Yanga -Iringa

    March 25-30 ASFC robo fainali

    ReplyDelete
    Replies
    1. NANI HAPO ANA NAFUU ? AFADHALI YANGA RATIBA YAKE INA SIKU ZA KUPUMUA KULIKO SIMBA. TUCHEZENI TUU HIYO NDIYO LIGI HAKUNA KULALAMIKA

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic