February 7, 2019


Baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Yanga dhidi ya Singida United ya mjini Singida, Kocha Mwinyi Zahera amefunguka tena kuhusiana na ratiba ya ligi.

Zahera ameeleza hakika ratiba imekuwa si rafiki kwao ukiangalia kumekuwa na changamoto ya usafiri kutumia umbali mrefu wakiwa kwenye gari.

Zahera amesema wanapatwa na uchovu kwani tena wanapaswa kurejea Tanga kwa ajili ya mechi dhidi ya JKT Tanzania.

Amewataka Bodi ya Ligi kupitia TFF kuwa wanapaswa kujipanga kwakuwa wachezaji wake wanachoka na wanaweza wasihimili mikimikiki ya ligi kwasababu wanakuwa wanatumia nguvu nyingi.

Katika mchezo huo wa jana, Yanga ililazimishwa suluhu ya bila kufungana na ukiwa na mchezo wake wa pili ikikosa alama mbili baada ya Coastal Union ambayo walienda nayo sare ya 1-1.


5 COMMENTS:

  1. Acha kuzingua hivi kweli hukujua sio rahisi kuvuna point uwanja usio wako....mbona alilalamikia ratiba ya awali kabisa ambapo mechi tatu za Yanga ilikuwa ianze nje ya Dar! Ratiba imebana kwa kila timu .

    ReplyDelete
  2. hatua ni ngumu hasawa kwatimu kama yanga maana watu wa mikoani hukamikia timu kubwa tena ukizingatia hutua hii ya lala salama hivyo yanga wakubaliane matokeo.

    ReplyDelete
  3. Acha kelele Zahera, kwani hela za kupandia ndege kwasasa hakuna? kumbe mlikuwa mnajisifu kupanda ndege kwavile mechi zile za Mwadui na Kagera mlishinda? Tafuteni nauli za ndege mkiona wachezaji wanachoka kwenye mabasi. Acha visingizio, Yanga haijaumbwa kushinda tu.

    ReplyDelete
  4. Kwan timu nyingine wao hawasafiri ? Mbona hawalalamiki?

    ReplyDelete
  5. Hizi hapa ratiba za Simba na Yanga kwa mwezi huu Februari 2019

    SIMBA SC

    ��07/02/2019
    Simba vs Mwadui - Dar

    ��12/02/2019
    Simba vs Al Ahly - Dar

    ��16/02/2019
    Yanga vs Simba - Dar

    ��19/02/2019
    Africa Lyon vs Simba - Arusha

    ��22/02/2019
    Azam vs Simba - Dar

    ��26/02/2019
    Lipuli vs Simba - Iringa

    ��03/03/2019
    Stand United vs Simba - Shinyanga

    ��09/03/2019
    Js Saoura vs Simba - Algeria

    ��16/03/2019
    Simba vs As Vita - Dar

    ��18/03/2019
    Simba vs Ruvu Shooting - Dar

    ��31/03/2019
    Simba vs Mbao - Dar

    YANGA SC

    ��06/02/2019
    Singida United vs Yanga -Singida

    ��10/02/2019
    JKT Tanzania vs Yanga -Tanga

    ��16/02/2019
    Yanga SC vs Simba -Dar

    ��20/02/2019
    Mbao vs Yanga -Mwanza

    ��25/02/2019
    Namungo vs Yanga -Lindi

    ��02/03/2019
    Alliance School vs Yanga Mwanza

    ��10/03/2019
    Yanga vs KMC -Dar

    ��16/03/2019
    Lipuli FC vs Yanga -Iringa

    March 25-30 ASFC robo fainali

    HAPO NANI WA KULALAMIKIA RATIBA KATI YA SIMBA NA YANGA??? AFADHALI YANGA INA NAFUU. KAZENI BUTI LIGI HIYO.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic