February 12, 2019


Ni kama hakuna haja ya kusafiri kwenda mkoani tena ama Zanzibar kama ilivyozoeleka kwa kikosi cha Simba ambapo kuelekea mechi dhidi ya watani wa jadi Yanga, kitakuwa hapahapa Dar es Salaam.

Ikumbukwe mara ya mwisho katika mchezo ambao ulimalizika kwa suluhu ya bila kufungana, Simba ilifanya maandalizi yake kwenye Uwanja wa Boko Veterani na kuahirisha safari ya kwenda visiwani Zanzibar.

Simba haitoweza kusafiri kwenda popote kwani itakuwa na siku chache baada ya mchezo wa leo dhidi ya Al Ahly kumalizika Dar es Salaam.

Wekundu hao wa Msimbazi wanakabiliwa na mechi hiyo kubwa ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo watapaswa kupambana kusaka alama tatu ili kujiwekea nafasi nzuri ya kufika hatua ya robo fainali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic