February 12, 2019


Homa ya watani wa jadi, Simba na Yanga imezidi kushika kasi ambapo kikosi cha Yanga kimeamua kutofika kabisa Dar es Salaam na badala yake kimeweka kambi Morogoro.

Yanga imeamua kuishia Morogoro kikitokea Tanga na kuweka kambi maalum kujiandaa dhidi ya Simba ambapo timu hizi zitakutana Jumamosi ya wiki hii kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Tayari Kocha Zahera ameshaanza kuwapa tizi la maana vijana wake kuhakikisha kuwa wanapambana na kuchukua alama tatu dhidi ya Simba ambao nao wanapigania kutetea taji la ligi.

Kambi hiyo inawafanya Yanga washindwe kuwashuhudia Simba Uwanja wa Taifa ambapo watacheza dhidi ya Al Ahly leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba atakuwa anacheza kipute hicho cha Ligi ya Mabingwa Afrika na kisha baada ya hapo maandalizi dhidi ya Yanga yataanza.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic