March 15, 2019


LEO Singida United majira ya saa 1:00 usiku watashuka Uwanjani kumenyana na Azam FC wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wao uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar.

Kiongozi wa Singida United Dr. Mwigulu Nchemba, amesema kuondokewa na  wachezaji wengi kwenye timu yao na mabadiliko kwenye benchi la ufundi kumepelekea kushindwa kupata usawa wa kiushindani katika ligi.

"Mwaka jana Singida ilikuwa na msimu mzuri, ilimaliza katika nafasi 5 za juu kwenye ligi wachezaji wengi waliokuwepo mwaka jana mwaka huu hawapo kwa sababu mbalimbali wengine wakiwa wamepata sehemu nyingine. Sasa hivi timu imeanza kujengwa upya, sasa timu ikiwa inajengwa halafu ligi inaendelea madhara yake ndiyo ya namna hii.

"Tunachofanya sasa hivi ni kuhakikisha timu inaendelea kuwepo kwenye ligi lakini jambo lingine kule ambako tunaweza kuwa bingwa tutapambana tuwe bingwa." amesema Nchemba.

Singida United ipo nafasi ya 16 kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 33 baada ya kucheza mechi 28.

2 COMMENTS:

  1. We mwenyewe umegawa wachezaji yanga kwa ushabiki halafu unalalamika nn

    ReplyDelete
    Replies
    1. Enter your reply...hajui atendalo asubiri kushuka daraja aukimbie uboss wa timu

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic