May 6, 2019


KOCHA Mkuu wa Mbao FC, Salum Mayanga na msaidizi wake, Novatus Fulgence wametumia dakika 270 kupata pointi tatu, baada ya kukabidhiwa timu mwezi Marchi mwaka huu wakichukua mikoba ya Ally Bushir.
Mayanga alianza kazi kwa kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Simba mchezo uliochezwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro, akapoteza mbele ya Biashara United Uwanja wa  CCM kirumba kwa kufungwa bao 1-0 kabla ya kutoka suluhu na Azam FC ya Dar uwanja wa CCM kirumba.
Juzi alivuna pointi tatu mbele ya Ndanda uwanja wa CCM Kirumba baada ya kushinda mchezo wake wa kwanza kwa bao 1-0 lililofungwa na mshambuliaji Said Junior ambaye kwa sasa amefunga jumla ya mabao nane kwenye ligi.
Hivyo Mayanga ametumia dakika 270 kuvuna pointi tatu ambazo zimemuondoa kutoka nafasi ya 19 aliyokuwa akishika mpaka kufika nafasi ya  13 kwenye msimamo baada ya kucheza michezo 34 wamejikusanyia pointi 40. 

1 COMMENTS:

  1. Kocha wa taifa stars huyo? Kesho utasikia amekabidbiwa ngorongoro heroes?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic