KIKOSI cha Simba leo kimerejea kutoka mkoani Mbeya baada ya kucheza michezo miwili ya Ligi Kuu Bara.
Simba wamerejea na pointi sita na wamefunga jumla ya mabao matatu kwenye michezo yao miwili waliyocheza uwanja wa Sokoine na wameruhusu kufungwa bao 1 na Idd Naldo wa Mbeya City.
Ushindi huo umeifanya Simba kufikisha jumla ya pointi 78 ikiwa nafasi ya pili, mchezo wao unaofuata ni dhidi ya Coastal Union, uwanja wa Taifa, Mei 8.
Simba na Azam kuwakilisha nchi mashindano ya mwakani....nadhani ni afya kwa soka letu.....Simba analitwaa kombe mara mbili mfululizo!
ReplyDeleteHii nzuri
Delete