July 2, 2019



BAADA ya kocha wa timu ya KMC, Jackson Mayanja kupewa kandarasi ya mwaka mmoja ndani ya kikosi hicho ambacho kitashiriki michuano ya kimataifa msimu ujao amepewa jukumu la kumleta msaidizi wake kwenye benchi la ufundi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mayanja amesema kuwa anajua kwamba anawatambua makocha wengi wenye uzoefu hivyo atafanya nao mawasiliano kwa ukaribu kwa kushirikiana na uongozi wa KMC ili kupata kilicho bora.

“Mpango wangu mkubwa ni kumleta msaidizi makini ambaye tutafanya naye kazi kwa kushirikiana, kwa sasa tayari nimepewa baraka na uongozi hivyo ni muda wangu kutafuta mtu wa kufanya naye kazi kwenye benchi la ufundi,” amesema Mayanja.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic