July 2, 2019



IMEELEZWA kuwa mshambuliaji wa Mwadui FC, Salim Aiyee ameipasua timu yake kwa sasa kutokana na kusepa kwake  na kujiunga na KMC na kukikacha kikosi cha Mwadui ambacho ni miongoni mwa timu 20 zitakazoshiriki Ligi Kuu Bara.

Habari kutoka ndani ya Mwadui FC zimeeleza kuwa tayari uongozi wa Mwadui FC umeanza mazungumzo na nyota wa Mbao FC Said Jr ili kuziba pengo la Aiyee.

“Mwadui kwa sasa wanahaha kumpata mbadala wa Aiyee ambaye msimu ujao atakipiga KMC, hesabu zao ni kumpata mshambuliaji mwingine atakayeziba pengo lake na jicho kubwa kwa sasa lipo kwa Said Jr wa Mbao FC,” kilieleza chanzo hicho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic