July 16, 2019

UONGOZI wa Simba umesema kuwa ni kweli unadaiwa na mchezaji wao Juuko Murshid anayecheza timu ya Taifa ya Uganda ila haina mpango wa kuachana naye kizembe.

Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori amesema kuwa, Murshid ni mtoro wa timu anapaswa arejee haraka kabla ya kuchukuliwa hatua.

"Tunadaiwa na Murshid mshahara wa miezi miwili, haina maana tunashindwa kumlipa hapana, yeye ametoroka kambini hivyo hauwezi kumlipa mshahara mfanyakazi mtoro.

"Kwa sasa popote alipo anatakiwa arejee kazini akishindwa tutamchukulia hatua mpaka Fifa kwa kuwa tumemuandikia barua hajatujibu, hivyo tunalishughulikia suala hilo kwa ukaribu," amesema.

4 COMMENTS:

  1. Lipeni mishahara ya dogo acheni Siasa.

    ReplyDelete
  2. kelele nyingi kumbe masikini wakubwa nyieee

    ReplyDelete
  3. Wacha ujinga. Mchezaji mtoro alipwe?Toroka wewe lakini halafu ulipwe. Akira ni ajira haijalishi umeajiriwa wapi.Kuhusu umaskini ficheni aibu yenu.Bakuli lini tena?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic