UONGOZI wa
KMC, umeamua kutumia mtindo wa Simba katika kuhamasisha mashabiki wake kuelekea
kwenye mchezo wa kimataifa wa kombe la Shirikisho dhidi ya AS Kigali ya Rwanda
unaotarajiwa kuchezwa uwanja wa Taifa kati ya Agosti 23-25 kwa kuja na kauli
mbiu ya ‘Together we Can’.
Simba msimu uliopita kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa walikuwa wanatunga kaulimbiu maalumu kwa ajili
ya hamasa huku ile ya 'Yes We Can' ikiwa ni moja ya iliyobamba na zilikuwa
zinatambulishwa na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara.
Akizungumza
na Salehe Jembe, Ofisa Habari wa KMC, Anwari Binde amesema kuwa wameamua
kuja na kauli mbiu ili kuongeza hamasa na nguvu ya mashabiki kuelekea kwenye
mchezo wa marudiano.
“Utakuwa ni
mchezo mgumu na tayari kikosi kimeanza mazoezi kujiaandaa kuwavaa AS Kigali,
tumeamua kuja na kaulimbiu ya ‘Together we Can’
ili kuongeza hamasa na nguvu kwa mashabiki kuelekea kwenye mchezo wetu.
“Ombi letu
mashabiki wajitokeze kwa wingi washuhudie namna wachezaji watakavyotoa
burudani na kuwapa furaha kwa kupata matokeo chanya kwani kila kitu
kinawezekana,” amesema Binde.







0 COMMENTS:
Post a Comment