September 29, 2019



UONGOZI wa Kagera Sugar umesema kuwa kupoteza kwao mbele ya Simba sio mwisho wa ligi watakaza kwenye michezo yao yote iliyobaki ikiwa ni pamoja na wa leo dhidi ya JKT Tanzania.

JKT Tanzania inakaribishwa leo na Kagera Sugar ikiwa imetoka kushinda mbele ya Biashara United bao 1-0 huku Kagera Sugar wao wakiwa wamejeruhiwa na Simba kwa kufungwa mabao 3-0.

Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Maxime amesema kuwa wameachana na maumivu ya kupoteza mbele ya Simba sasa wanazitaka pointi tatu za JKT Tanzania.

“Tumepoteza mchezo wetu uliopita haina maana kubaki kuufikiria sasa tunahitaji kuona tunapata matokeo mbele ya wapinzani wetu hakuna namna nyingine,” amesema.

Mohamed Abdallah ‘Bares’ Kocha wa JKT Tanzania, amesema kuwa wamejipanga kuendeleza furaha ya mashabiki wa JKT Tanzania watacheza kwa tahadhari kupata ushindi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic