October 1, 2019



HALI inazidi kuwa moto ndani ya Singida United baada ya kupigwa chini kwa aliyekuwa Kocha Mkuu Felix Minziro mpaka sasa imetumia dakika 450 kusaka pointi mbili pekee.

Singida United imecheza jumla ya michezo mitano ndani ya Ligi Kuu Bara inayodhaminiwa na Vodacom haijapata ushindi kwenye michezo hiyo zaidi ya kuambulia sare pekee.

Ilianza kupoteza mbele ya Mwadui FC kwa kufungwa bao 1-0, ikapoteza mbele ya Namungo FC kwa kufungwa mabao 2-0,ikalazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Ndanda FC pia ikalazimisha sare ya 0-0 na Mbao FC kabla ya kupoteza mbele ya Alliance kwa kufungwa bao 1-0.

Kwenye michezo mitano iliyocheza mpaka sasa imefunga jumla ya bao 1 na imefungwa mabao matano yanayoipa pointi mbili.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic