SELEMAN Mataso, Mwenyekiti wa Biashara United
amesema kuwa wanawatambua vema Yanga hivyo watapambana kupata pointi tatu
muhimu kwenye mchezo wao wa kesho wa ligi utakaochezwa uwanja wa Uhuru.
Biashara
United itamenyana na Yanga, Desemba 30 ikiwa ni mchezo wao wa 12 ipo nafasi ya
15 ikiwa na pointi 15 wapinzani wao Yanga wapo nafasi ya tatu baada ya kucheza
mechi 10 na wana pointi 21.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Mataso amesema kuwa wanautambua mfumo wa Yanga jambo ambalo
haliwapi shida wana imani watawapa taabu watakapokutana kwenye mechi hiyo.
“Tunatambua
kwamba wameshinda mbele ya Tanzania Prisons ila hiyo haiwapi nafasi kututisha
nasi kwenye mchezo wetu lazima tutawape taabu na hesabu zetu ni kupata pointi
tatu muhimu,” amesema Mataso.
Sawa endeleeni kuikamia Yanga mwisho kitawakuta kilichowakuta Stand United. KMC: Mbeya City ; Ruvu Shooting wameshangilia kupata matokeo kwa wana wakajiona wamemaliza ligi sasa wanapumulia mashine
ReplyDeleteUnawatisha wawaachie. Chezeni mpira. Hakuna kushinda kwa jina. Mpira uwanjani.
ReplyDeleteManeno mengi ya nini?,goli 2tuu Zina wa subiri mbele yetu
ReplyDelete