UONGOZI wa
Coastal Union umesema kuwa upo sokoni kutafuta majembe matatu ya kazi ili
kuongeza ukali wa kikosi hicho chenye ngome yake mkoani Tanga.
Coastal
Union ipo nafasi ya sita baada ya kucheza mechi 13 imejikusanyia jumla ya
pointi 20 itacheza kesho na Mbeya City uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Akizungumza
na SpotiXtra, Kocha Mkuu wa Coastal Union, Juma Mgunda alisema kuwa hesabu
kubwa kwa timu ni kuongeza nguvu kwa kusajili wachezaji watatu ambao wataongeza
kasi ya ushindani.
“Kila timu
inafanya usajili kulingana na mahitaji yake, kwa namna kikosi chetu kilivyo
hakihitaji maboresho makubwa kwani wachezaji wake wengi wameanza kuzoeana na
kufanya kazi kwa ukaribu nitaongeza wachezaji watatu pekee.
“Nafasi zote
zina wachezaji ambao nawaamini ila nikipata mshambuliaji mmoja, kiungo
mshambuliaji na mkabaji hapo kikosi kitakuwa kwenye ubora wake, ila
ikishindikana nitapandisha vijana wangu wa timu ya vijana,” alisema Mgunda.
0 COMMENTS:
Post a Comment