December 31, 2019



UONGOZI wa Ndanda FC umesema kuwa utatibua rekodi  mabingwa watetezi Simba iliyo nafasi ya kwanza na pointi 31 baada ya kucheza mechi 12 ikiwa chini ya Sven Vanderbroek ambaye ameongoza mechi tatu bila kufungwa akiwa kwenye benchi.

Sven raia wa Ubelgiji alichukua mikoba ya Patrick Aussems aliyetimuliwa ndani ya Simba ameanza kwa kasi ambapo kwenye jumla ya mechi tatu za mwanzo sawa na dakika 270 hajafungwa zaidi ya kujikusanyia mabao 12 atamenyana na Ndanda leo, Desemba,31 uwanja wa Taifa.

Simba ikiwa chini ya Sven alianza kuiongoza kwenye mechi dhidi ya Arusha FC iliyokuwa ya Kombe la Shirikisho na ilishinda mabao 6-0, kwenye mechi mbili za ligi kuu mbele ya Lipuli ilishinda mabao 4-0 pia ilishinda mabao 2-0 mbele ya KMC mechi zote zilichezwa uwanja wa Uhuru.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Ndanda FC iliyo nafasi ya 19 na pointi nane, Idrisa Bandari amesema kuwa kikosi kipo imara hakitishwi na rekodi zinazowekwa na mtu yoyote zaidi ya kupigia hesabu pointi tatu.

“Maandalizi yetu sisi siku zote ni kuona kwamba timu inapata matokeo chanya na kushinda bila kuangalia rekodi ambazo zinawekwa, hakuna kinachotuogopesha kwa wapinzani wetu tutapambana kupata pointi tatu muhimu mbele ya Simba,” amesema Idrisa.


1 COMMENTS:

  1. Tuliahidi kutibuwa kama wanavoahidi wa Jangwanic lakini tukatibuliwa na wa jadi wanaombwa kuroweka nywele kwa sabuni ili uwembe usiikekete kichwa

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic