Inaelezwa kuwa mabosi wa klabu ya Simba wamesema wapo mbioni kukamilisha usajili wa straika kutoka Mamelod Sowndowns ya Afrika Kusini anayecheza kwa mkopo UD Songo ya Msumbiji, Luis José Miquissone
Taarifa zinasema Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Senzo Mazingisa amesema wako mbioni kukamilisha usajili wa mchezaji huyo.
Kwa mujibu wa bosi huyo, ameeleza hadi sasa hawajafanya usajili wowote wa mchezaji tangu kufunguliwa kwa dirisha dogo.
Aidha, Mazingisa ameeleza kuwa usajili wtaakaoufanya utakuwa ni kwa madhumuni ya mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika na si kuelekea mechi ya watani wa jadi dhidi ya Yanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment