January 8, 2020



ADEYUM Suleiman, beki wa kushoto wa Yanga alitumia dakika 45 tu kuiondoa jumla timu ya Jamhuri, kwenye mbio za kuwania Kombe la Mapinduzi linalofanyika Visiwani Zanzibar, baada ya kufunga bao la kwanza kwenye ushindi  wa mabao 2-0 waliyopata Yanga.

Bao la kwanza alilifunga Adeyum kwa mpira wa adhabu akiwa nje ya 18 kwa kupiga shuti kali lililozama moja kwa moja langoni huku likimuacha mlinda mlango wa Jamhuri akilisindikiza kwa macho dakika ya 45.

Kuingia kwa Mohamed Issa ‘Mo Banka’ dakika ya 79 akichukua nafasi ya Mapinduzi Balama kuliongeza kasi ya mashambulizi ambapo kiungo huyo alitumia dakika sita kuifungia timu yake bao lake la pili .

Mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Amaan, ulikuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote kupambana kutafuta matokeo ila bahati haikuwa kwa Jamhuri kwani uimara wa mlinda mlango wa Yanga, Ramadhani Kabwili uliwazuia kupata mabao.

Yanga sasa inatinga hatua ya nusu fainali inayotarajiwa kuchezwa Ijumaa, Januari 10, Uwanja wa Amaan dhidi ya Mtibwa Sugar ambayo ilishinda mbele ya Chipukizi kwenye mchezo wa robo fainali baada ya sare ya kufungana bao 1-1 ndani ya dakika 90 na Mtibwa Sugar ilishinda kwa penalti 4-1.

Kwa ushindi wa Yanga unafanya timu zote za Visiwani Zanzibar msimu huu kuishia kwenye hatua ya robo fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya Mlandege kutolewa na mabingwa watetezi Azam FC  itakayomenyana na Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic