January 10, 2020


KOMBE la Mapinduzi linazidi kuchanja mbunga taratibu kueneleka kumtafuta bingwa wa mwaka 2020.

Tayari timu zimeanza kujiengua ambapo tangulianze kumtafuta mbabe wake huko visiwani Zanzibar, Januari, 6,2020 tayari wengine wameshajiengua.

Azam FC ilianza kukata tiketi ya kutinga hatua ya nusu fainali kwa kushinda mbele ya Mlandege kwa bao 1-0 kisha Mtibwa Sugar ilitinga hatua ya nusu fainali kwa ushindi wa penalti 4-1 mbele ya Chipukizi baada ya dakika tisini ngoma kuwa sare ya bao 1-1.

Kwa upande wa Yanga wao wameshamaliza kete zao baada ya kuanza robo fainali vema mbele ya Jamhuri kwa ushindi wa mabao 2-0 kabla ya kutolewa na Mtibwa Sugar kwa changamoto ya penalti 4-2 baada ya dakika tisini kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1.

Ni aina ya michuano ambayo ipo katikati ya Ligi Jambo linalofanya Ligi isimame kwa muda kulingana na shughuli nzima ya michuano hii ambayo hufanyika kila baada ya mwaka mmoja kwa baadhi ya timu ambazo zinashiriki.

Timu zinazoshiriki zilikuwa nane safari hii na zote ni za Tanzania tofauti na zamani ambapo kulikuwa na waalikwa ambao walikuwa wanakuja kunogesha mashindano haya ambayo yana heshima yake.

Ukiachana na kutokuwa kwenye kalenda ya Fifa bado ni miongoni mwa mashindano ambayo yamekuwa yakikuza na kukomaza viwango vya wachezaji ambao walikuwa hawapati nafasi ya kuonyesha kile ambacho wanacho.

Mashindano yanatoa fursa ya kutambua uwezo wa wachezaji husika wa timu moja na kurahisisha kazi kwa mwalimu katika kupanga kikosi kazi ambacho atakitumia wakati wa mashindano mengine nje ya Mapindizi yenyewe ambayo hayachukui muda mrefu.

Kutokana na sababu hiyo wengi wamekuwa wakiyapuuzia na kuchukulia ni mashindano ya kawaida ila ukweli ni kwamba si kama ambavyo wanafikiria yana umuhimu wake kuwepo ndani ya ardhi ya visiwani Zanzibar.

Miongoni mwa sababu zinazofanya yawe na umuhimu kwa kuwa inafanya muunganiko  uzidi kuwa imara kutokana na kushirikiana katika masuala ya kitaifa na kutufanya tuzidi kuwa na umoja.

Sisi site ni ndugu na tunapozidi kuwa karibu tunaongeza ukaribu wetu na undugu wetu kwa nchi ambayo inasifika kwa amani na upendo itazidisha kuujenga upendo kwa ndugu na wengine ambao bado wapo kwenye muungano kwa muda mrefu.

Wachezaji wote ninapenda kuwaambia kwamba ishu ya Mapinduzi sio muda wa kucheza kwa kukomoana hii sio sawa ni vema mpira wa kiungwana ukachezwa na kila mmoja akafanya vema kwa kipaji alichopewa na Mungu.

Kazi ya usalama wenu mkiwa ndani ya Uwanja ipo mikononi mwa wachezaji ni muhimu kulizingatia hilo na kulifanyia kazi kwa wakati kabla ya kuanza kuendelea kutafutiana visasi visivyo na maana.

Ikumbukwe kuwa mchezaji akipata majeruhi wakati huu itamfanya akose mechi kutokana na kuwa bize kutibu majeraha yake hili jambo linaumiza hasa ukizingatia ni ndani ya wiki moja Ligi itaendelea.

Ninachokiona ni kwamba mlinzi wa kwanza kwenye haya mashindano ni mchezaji. Jukumu kubwa la kucheza kwa umakini bila kusahau kucheza soka linaloeleweka uwanjani.

Uwepo wa mashabiki ambao watatupa keki ya uwanjani ni muhimu wakajilinda wenyewe na kufanya kazi ya kutoa burudani kwa mashabiki ambao wameshaanza kutoka makwao na wengine wakijiandaa kuja kuitazama.

Kila timu isikubali kuonyesha ubabe ila kwa namna makundi yalivyo na ushindani ulivyo ni imani yangu kwamba kila mchezaji ana kazi ya kuwa mlinzi wa mchezaji mwenzake ndani ya uwanja ili kumfanya awe salama muda wote.

Mgawanyo wa makundi pia mawili unatoa picha kwamba ushindani utakuwa mkubwa na rai yangu kwa wachezaji katika hali ya kawaida itawafanya wawe bora.

Mtindo wa kuchezeana rafu ndani ya mechi na kisha kutafuta sababu na kuomba msamaha hii haileti afya kwenye kazi ya soka letu kikubwa wachezaji wanatakiwa kuwa makini wawapo ndani ya Uwanja.
.
Mpira wa miguu una purukushani kwa sasa ndani ya uwanja ila haitoi fursa kwa wachezaji kucheza rafu ambazo hazina maana kwa wachezaji itawaumiza wachezaji wengine.

Ulinzi wa mchezaji na afya ya mchezaji ni muungano mzuri utakaofanya mapinduzi bora kwenye soka letu la Bongo kiujumla kwani amani itatawala.

Itakuwa furaha kuona namna mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam FC wakikutana na ushindani na wakatoa burudani bila wachezaji kuchezeana rafu sizizo na maana itapendeza.

Kila kitu kinawezekana ni suala la kukubali na kujituma kwa wachezaji wetu huku wakiongeza umakini maradufu wawapo ndani ya uwanja kutimiza majukumu yao ipasavyo. Nina imani hawatatuangusha katika hili.

Mashabiki kazi yenu ni moja kuleta shangwe muda wote na sio kusubiri chenga ama goli hapana hii si nzuri ni mwaka mpya na habari nyingine zinapaswa zifanywe kwa utofauti.

Shangilia ya mashabiki itaongeza utamu wa Mapinduzi na kila mmoja akitimiza jukumu lake itafanya kazi kuwa bora na kila mmoja kufurahi kupata burudani, kila la kheri wachezaji pamoja na mashabiki tunahitaji kuona bingwa bora anapatikana.

Timu shiriki zinapaswa zionyeshwe maana halisi ya kushindana kwa kutoa burudani na kucheza kwa juhudi bila kujali aina ya timu ambazo wanakutana nazo.
Wachezaji wengi huwa wanatatzio la kudharau mechi jambo ambalo halipaswi kutokea kwenye maisha ya soka letu kwani dakika tisini ndizo zenye majibu sahihi ya kile unachokitafuta.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic