January 10, 2020






 KWA sasa kila mmoja anacho kile ambacho alikuwa akijenga picha kwa muda wa miezi kadhaa nyuma ambapo kila mmoja alikuwa anavutia upande wake kwa kile alichoamini ni bora.

Simba na Yanga hapa ndio nazungumzia baada ya kucheza mchezo wao wa kwanza kwa msimu wa 2019/20, January 4,2020, balaa lilikuwa ni kubwa uwanjani na mwisho wa siku mbabe hakuna kati yao kwa sasa zile tambo zimepungua.

Leo sitapenda kuzungumzia matokeo kwani kila mmoja anatambua kuwa ilikuwa sare ya kufungana mabao 2-2 pale uwanja wa Taifa kwa hilo inatosha kujua kwamba hizi timu zinajuana na zina historia kwa muda mrefu.

Kidogo tu naweza kugusia kwa kuwapa pongezi wachezaji wa Yanga Kwa kuonyesha ukomavu wao mwanzo mwisho bila kukata tamaa licha ya kuwa nyuma kwa kufungwa mabao mawili na watani zao Simba ambao walipania kushinda.

Ukweli ni kwamba kilichowapa nguvu ya kupambana Yanga ni ile nguvu waliyokuwa nayo na sapoti kutoka kwa mashabiki walionyesha nidhamu ya soka kwa kutulia na kuwaheshimu wapinzani wao.

Kwa upande wa Simba hili linapaswa liwe fundisho hawapaswi kudharau timu pinzani hata wakiwa mbele kwa mabao matano kabla mpira haujaisha kwani kilichotokea baada ya kufungwa bao moja walipoteza matumaini na kuanza kucheza bila kujali wanafanya nini.

Walisahau majukumu yao uwanjani na wakaruhusu kuanza kumtafuta mchawi nani ndani ya uwanja wakati mpira unaendelea na hakuna ambaye alikuwa anajali jambo hili hiki kiliwavuruga Simba .

Inaonesha kuwa ndani ya Simba kwa sasa kila mchezaji ni mkubwa kuliko mwenzake hakuna anayetaka kumsikiliza mtu mwingine zaidi ya kufanya kile anachokiamini hili halipo sawa na kama ni utamaduni mpya unapoteza ladha na asili ya Simba na mpira kiujumla.

Mpira hautoi muda wa kuanza kumtafuta mchawi wakati bado kuna muda wa kupambana badala yake unatoa muda wa kurekebisha makosa na kuongeza mshikamano mwanzo mwisho.

Nimeamua niligusie kidogo kwani likifumbiwa macho kwa sasa litakua tatizo kubwa ambalo litafuta mazuri yote ya wachezaji ndani ya timu pamoja na uongozi kiujumla.

Pia mashabiki kwa kujitokeza uwanjani nawapa pongezi wote si wa Simba wala Yanga uwanja ulipendeza na hamasa ilionekana mwanzo mwisho ndani na nje ya uwanja wa Taifa.

Hiki ndicho ambacho kinatakiwa kifanyike siku zote na kuendelea kuona ni namna gani mambo yanaweza kubadilika ndani ya mwaka 2020 kwenye suala la ushangiliaji na kujitokeza uwanjani.

Simba walikuwa wanyonge baada ya matokeo na hii ilitokana na kujiamini kupiga kiasi wakiwa ndani ya uwanja kwa hili linapaswa lifanyiwe kazi pia na benchi la ufundi pamoja na uongozi kiujumla ujue ni namna gani unaweza kurudisha ari ya timu.

Kwa mwenendo walionao kwa sasa endapo wataendelea namna hii na kujiachia wakiwa uwanjani mambo yatakuwa tofauti na vile ambavyo wanafikiria kwani wachezaji walionyesha kukubali matokeo waliyoyapata.

Morali ya timu inapaswa ijengwe upya na iishi muda wote ndani ya dakika tisini mpaka mwamuzi atakaposema sasa inatosha na kupuliza kipyenga chake cha mwisho na sio kabla timu inapoteza ushirikiano.

Yanga nao wanakazi ya kufanya licha ya kuonekana wao wamekuwa wababe kurudisha mabao yao wasisahau kwamba ligi bado haijakamilika mambo yanaendelea.

Rai yangu kwa mashabiki siku zote wanapokwenda uwanjani wasiwe na matokeo yao mfukoni litawakosesha raha siku zote bali wanapaswa watambue kuwa kazi ya matokeo ni ndani ya Uwanja kwa wachezaji wenyewe.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linapaswa litazame namna bora ya kuwavuta mashabiki kwenda uwanjani kuzipa sapoti timu zao na kuona namna gani zinafikia malengo ya kuongeza hamasa kwa mashabiki.

Ilivyokuwa Simba na Yanga ikipewa promo basi uwe pia hata wakati KMC itacheza na Ndanda kwa kutoa taarifa mapema na kuangalia mambo ambayo yatawaweka karibu wachezaji.

Sapoti na nguvu kubwa kwa mashabiki na TFF inapaswa iendelee siku zote bila kufikiria ni timu ipi ambayo inacheza kwenye mechi zao za ligi pamoja na za mashindano mengine.

Hali hii ya kuzipa sapoti timu zetu isiishie kwenye ligi tu inapaswa izidi kuendelea muda wote katika kazi na kuendelea kushuhudia ligi ikizidi kupamba moto.

Mashabiki ni muhimu kuendelea kutoa sapoti kwa timu zote kwa kuwa mpira unahitaji sapoti na kuna namna gani wachezaji watafanya kazi zao ndani ya uwanja.

Kwa wachezaji pia iwe somo kujifunza kupitia makosa na kufanya kazi kwa juhudi ndani ya uwanja bila kujali aina ya timu ambayo unacheza nayo.


3 COMMENTS:

  1. Jana vipi kuna alieenda na matokeo uwanjani huko Zanzibar?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJanuary 10, 2020 at 2:01 PM
    Yanga walijua watapenya kwa urahisi.Wakijua kwamba wanaweza kupambana na Simba waliamua kupumzisha wachezaji wa kikosi cha kwanza..Yondani aliingia toka benchi baada ya kuwa tayari wamefunga.Lamine aliendelea kubaki benchi...Haruna na Sibomana hawakuwepo.Golini alikaa kipa namba tatu.Lengo kikosi cha kwanza kiwe fiti ili kucheza mchezo wa nguvu na rafu kama ilivyokuwa kwa Prison na Simba.Wakatunguliwa sekunde ya mwisho gemu plan ikaanza upya.Kikawa kisingizio toka kwa Nungaz eti wamekuja kushindana sio kushinda na kuwa hawakulitaka kombe lisije waumizia wachezaji!Sasa sijui kombe gani wana uhakika nalo...la FA au la Premium league

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic