January 12, 2020



SAID Ndemla ni miongoni mwa wachezaji wazawa ndani ya Simba ambaye amekuwa na nafasi finyu ndani ya kikosi hicho licha ya kuwa na uwezo mkubwa kwenye miguu yake na akili za kufikiria.

Msimu uliopita akiwa chini ya Patrick Aussems aliweza kuonyesha makeke yake kiasi chake na kwenye mchezo dhidi ya KMC uliochezwa uwanja wa Taifa  alirudisha tabasamu lake kwa muda baada ya kufunga bao la kwanza kwenye mchezo huo akiwa nje 18.

Ugumu wa nafasi ndani ya Simba iliyo chini ya Sven Vanderbroek kwa sasa aliyepokea mikoba ya Aussems unatokana na kuwa na viungo wengi waliosajiliwa ikiwa ni pamoja na Clatous Chama, Hassan Dilunga, Ibrahim Ajibu, Francis Kahata na Sharaf Shiboub.

Baada ya dirisha dogo kufunguliwa timu nyingi zimekuwa zikimpigia hesabu ikiwa ni pamoja na Polisi Tanzania, Singida United na KMC ambao wanahitaji huduma yake, 

Huyu hapa Ndemla anaweka wazi kuhusu hesabu zake na mipango yake kwa sasa:-
“Hapa nilipo kwa sasa si kwa bahati mbaya bali inatokana na malengo ambayo ninayo kwenye kichwa changu na bado ninaendelea kupambana kuyafikia hayo malengo.

 Mipango inakwendaje?

“Kila siku mpya ninayoanza ninashukuru kwa Mungu na kuitazama kuwa ni siku yangu ya mafanikio kwa kufikiria vitu vipya vya kufanya ambavyo vitanifanya nifikie malengo makubwa.

Singida United na Polisi zinahitaji saini yako hili lipoje?

“Kwangu mimi kunipata itakuwa ngumu hasa ukizingatia kwamba kwa sasa nina mkataba na timu yangu sasa sijui wao wananitaka kwa nini ila kwa kuwa ni mchezaji basi nipo ndani ya Simba.

Unapenda kuitumikia timu gani?

“Hakuna timu ninayoifikiria zaidi ya Simba, naskia Singida United wanasema ninaweza kuikoa isishuke daraja, hili si kweli sina uwezo huo wa kuinusuru timu isishuke daraja ni timu inayocheza na si mchezaji mmoja.

Ushindani wa namba  unauzungumziaje?

“Kama sehemu hakuna ushindani huwezi kuwa bora, ila kwa kuwa nakutana na ushindani huu ni kawaida kwa mchezaji duniani kote hili suala lipo.

“Kuhusu suala la kuanza halipo mikononi mwangu anayepanga kikosi ni kocha mwenyewe yeye ndiye anayejua aina ya wachezaji anaowataka waanze.

Nafasi yako ipoje?

“Bado nipo Simba na nina mkataba na Simba hiyo ndiyo nafasi yangu.

Unajiona wapi miaka mitano mbele?

“Muda bado upo wa kupambana, najiona mbali kwani kipaji ninacho na uwezo Mungu amenipa.

Kwa nini Simba na si kwingine?

“Ndipo ambapo nipo na ni mabosi wangu kwa sasa ndio maana nipo hapa.

Dili lako la kwenda nje lipoje?

“Hilo kwa sasa siwezi kulizungumzia mambo yakiwa sawa litakuwa wazi.

Utakosa nini kwa Aussems?

“Kazi ya mchezaji ni kufanya kile anachoambiwa na kocha kuhusu kumkumbuka ana mengi ambayo tumefanya naye ila yatabaki ndani ya moyo wangu.

Unamzungumizaje kocha mpya?

“Kiukweli kwa mwanzo ambao tumeanza naye na namna ilivyo ni ngumu kumzungumzia kocha wetu mpya hata kumtofautisha na yule aliyepita siwezi kabisa kuzungumzia hilo lipo juu ya uwezo wangu.

Unawaambia nini mashabiki?

“Sapoti yao katika kila tunachokifanya ni muhimu kwani mafanikio yetu yanabebwa na mashabiki ambao wanatupa sapoti kila mara ambapo tunakuwa.

Ushindani ndani ya ligi unakupa kitu gani?

“Ushindani ni mzuri kwani inaonyesha kila timu imejipanga, hata sisi tumejipanga kupata matokeo chanya ili kufikia malengo ya timu kiujumla.

“Ubingwa ni hesabu zetu ndio maana kila mechi kwetu ni sawa na fainali.Ligi ni ngumu kila timu inaonyesha imejipanga ili kupata matokeo mazuri,” anamaliza Ndemla.


2 COMMENTS:

  1. Safi sana Said Ndemla .Sasa nafikiri huyu kanjanja atakuacha ufanye kazi.Kila mwezi haipati Ndemla Ndemla utafikiri anakulipa mshahara au ni kocha wa Simba Ganga yako kanjanja

    ReplyDelete
  2. Welldone wa jina langu.Piga kazi achana na hao wabubujaji.Keep it up.kila la kheyr ufikie malengo yako

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic