February 22, 2020



KOCHA Mkuu wa Biashara United, Francis Baraza ameweka wazi kwamba hawawaogopi wapinzani wao Simba.

Biashara United leo itakuwa na kazi mbele ya Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00 usiku.

"Kiukweli Simba ni timu nzuri lakini siwaogopi kwa kuwa ninapocheza ugenini nina mbinu zangu ambazo nazitumia jambo linalonifanya nijiamini, hivyo Simba wasitarajie kupata matokeo kirahisi.

"Ukiangalia mchezaji mmoja mmoja kwa Simba wana uwezo binafsi na mimi nimeandaa mbinu zangu ambazo naamini kabisa zitanisaidia kupata ushindi," amesema.

Biashara United ina kazi ya kulipa kisasi mbele ya Simba kwa kuwa mchezo wa kwanza walifungwa mabao 2-0..


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic