August 15, 2020


INAELEZWA kuwa  Larry Bwalya na Walter Bwalya wote raia wa Zambia wapo kwenye rada za kuibukia ndani Simba na Yanga.


Larry Bwalya  mwenye miaka 25 yeye ni kiungo mshambuliaji anakipigandani ya Ligi Kuu ya Zambia kwenye Klabu ya Power Dynamos anahusishwa kujiunga na Yanga na inaelezwa mazungumzo baina ya pande zote mbili yanaendelea vizuri.

Walter Bwalya  mwenye miaka 25 huyu ni mshambuliaji wa zamani wa Nkana FC (The Red Devils) kwa sasa anakipiga Ligi Kuu ya Misri kwenye Klabu ya El Gouna FC yeye anahusishwa kujiunga na Simba.

Kwa muda mrefu Bwalya amekuwa akitajwa kuibukia Simba ila kikazwo awali ilikuwa inatajwa kuwa ilikuwa ni dau kubwa ila kwa sasa mambo yanaelezwa kuwa safi kwa pande zote mbili kuelewana.

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela amesema kuwa wapo vizuri katika masuala ya usajili wana imani ya kuwa na kikosi bora cha ushindani.

 

3 COMMENTS:

  1. Unatuzuga unawaelekeza Simba kuhusu Larry Bwalya ambaye yupo na Yanga ????? Bwalya mwingine hamumuwezi kwa za MO ENERGy

    ReplyDelete
  2. LARRY BWALYA yupo dar kwa ajili ya mazungumzo ya kujiunga na Simba. Mwandishi wewe ni mmoja wa maadui wakubwa wa Yanga, umekuwa ukitumika kuwasajilia Simba kupitia mgongo wa Yanga, lengo lenu ni kuidhoofisha Yanga kwakuwa mna amini Simba imara itaonekana mbele ya Yanga iliyo dhaifu. Wewe ni mtu hasidi sana kwa Yanga sema hawajakushtukia tu.

    ReplyDelete
  3. Larry Bwalya ameshamalizana na Simba, amesaini mkataba wa miaka miwili. Simba wamefanya kweli wakati Yanga walikuwa wanadanganya tu kuwa wanafuatilia.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic