August 1, 2020


AWESU Awesu nyota mpya ndani ya Klabu ya Azam FC ambaye amesaini kandarasi ya miaka miwili kukitumikia kikosi hicho amesema kuwa ilikuwa ni ndoto yake kurejea kuitumia timu hiyo.

Kiungo huyo alikuwa anatajwa kuingia rada za Yanga ambao walipishana naye kidogo kabla ya kumalizana na Zawad Mauya ambaye amesaini dili la miaka miwili ndani ya Yanga hivyo malengo yake ya kutaka kureea kwenye klabu yake ya zamani ni sababu kwake kuipotezea Yanga.

Kiungo huyo ambaye alikuwa anakipiga ndani ya Kagera Sugar na kutupia jumla ya mabao saba kwenye mashindano yote aliwahi kuwa kwenye kituo cha Azam Academy kwa miaka miwili 2014-15. Kisha akijiunga na Madini ya Arusha,Mwadui FC, Singida United  na Kagera Sugar ni timu alizozitumikia kabla ya kurejea Azam FC

Awesu amesema kuwa:”Ilikuwa ndoto yangu kurejea ndani ya Azam tangu nilipoondoka niliweka nia ya kurudi hapa tena ndani ya moyo wangu, Azam ni moja ya klabu kubwa na bora hivyo ingekuwa ngumu kwangu kugoma kusaini.”

  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat' amesema kuwa nyota huyo ni pendekezo la kocha Arstica Cioaba ambaye anahitaji kuboresha kikosi chake kwa msimu ujao.

“Kwenye mapendekezo yake wapo nyota ambao tumeanza nao kufanya mazungumzo madili yakikamilika kila kitu kitawekwa hadharani,". 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic