August 20, 2020

 

HAWA ni marafiki wa kitambo sasa wanaendelea kuwa marafiki ndani ya timu zao mpya namna hii:-


Awesu Awesu v David Kissu 


Wote wapo zao Azam FC. Walikipiga pamoja Singida United msimu wa 2008/19, Kisu msimu uliopita alikuwa  Gor Mahia na Awesu alikuwa Kagera Sugar sasa wote wapo Azam FC.


Joash Onyango v Francis Kahata 


Wote ni raia wa Kenya, Kahata na Onyango ni washakji kutoka ndani ya timu ya Taifa ya Kenya, 'Harambee Stars' alianza kuibuka Kahata msimu wa 2019/20 kisha Onyango kamfuata mshikaji wake ndani ya Simba 2020/21.


Kapama, Materema na Ufudu


Nyota hawa walikuwa washkaji ndani ya JKT Tanzania msimu wa 2018/19,  msimu wa 2019/20 wakatengana Materema alibaki JKT Tanzania,  Ally Nassor,'Ufudu' aliibukia Mbeya City na Nassor Kapama akaibukia Kagera Sugar ila sasa wote wapo Kagera Sugar 


Bwalya v Chama


Ni washakji kutoka timu ya Taifa ya Zambia,' Chipolopolo' sasa wote wawili, Larry Bwalya na Clatous Chama wanaendeleza urafiki ndani ya Simba msimu wa 2020/21.


Kalambo na Peter Mapunda 


Aron Kalambo na Mapunda walikuwa washkaji ndani ya Mbeya City na sasa wapo pamoja ndani ya Dodoma Jiji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic