August 12, 2020

 UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa beki mpya aliyetambulishwa na Yanga Agosti 9 bado ana mkataba ndani ya timu hiyo yenye maskani yake Morogoro.


Kibwana amesaini dili la miaka miwili ndani ya Yanga ambayo ipo kwenye harakati za kuboresha kikosi kwa ajili ya msimu wa 2020/21 akibeba mikoba ya Juma Abdul ambaye hajaongezewa mkataba.


Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa Kibwana bado ni mali ya Mtibwa hivyo wanafuatilia ili wajue imekuaje mchezaji ametambulishwa Yanga.


Kifaru amesema:-"Shomari kijana mdogo ni mali ya Mtibwa Sugar bado ana mkataba ndani ya timu na inaonekana alidanganywa huko alikokwenda kwa kuwa haelewi hatma yake lakini sisi tunafuatilia kwa ukaribu.


"Siwezi kusema ana mkataba wa miaka mingapi ila ninachojua mimi ni mchezaji wa Mtibwa Sugar, ninawasiliana na mtu wa sheria ndani ya timu ili ajue mambo yatakuaje," amesema.


10 COMMENTS:

  1. Hawa Utopolo wanasajili mchezaji mwenye mkataba tena bila uoga kwani wanajua wata play offer mentality ili waonekane wanaonewa. Mtibwa chukueni hatua huu mchezo lazima uishe.

    ReplyDelete
    Replies
    1. We Mkia hilo limeshatolewa ufafanuzi. Yanga imefuata utaratibu imeongea na viongozi waandamizi wa Mtibwa. Kama hao viongozi hawajamuarifu huyo mseamaji wao hayo ni mambo yao, hayaihusu Yanga. Mwaka huu mtapata tabu sana. Zusha jingine.

      Delete
    2. Wee nyani kwani mwaka huu wa 2020 umeshaisha na unajisahaulisha na 4g?... endelea kusikilizia maumivu.

      Delete
  2. Hi ni kiki ya mbwa was Simba aka mbwa was mooooo ambao mnataka jaja jaja za Morrison ili msishushwe daraja .....mpaka itaeleweka tu

    ReplyDelete
  3. MTIBWA SUGAR WALIKUA WAPI SIKU ZOTE HIZI ? HIZI NI NJAMA ZA SIMBA ILI YANGA IONEKANE INASAJILI WACHEZAJI WALIO NA MIKATABA NA CLUB ZAO !! WANADHANI WATANZANIA HAWANA AKILI AU HAWAJUI KUZICHAMBUA NJAMA ZAO!!! AZAM WALIISIFIA YANGA KUWA WAMEFANYA UUNGWANA KUWATAARIFU KUA WANAMTAKA SURE BOY NA LEO HAO HAO AZAM WANAILAUMU YANGA !!! MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA NA MWISHO WA SIKU MBIVU NA MBICHI ZITAJULIKANA TU

    ReplyDelete
    Replies
    1. Huyo Tobias Kifaru anakurupuka. Yanga imefuata utaratibu imeongea na viongozi waandamizi wa Mtibwa. Kama hao viongozi hawajamuarifu huyo mseamaji wao hayo ni mambo yao, hayaihusu Yanga.

      Delete
  4. wapuuuzi bhanaa
    kilaa upuuuzi waufanyao lazma waitaje Simba
    sasaa hapo Simba kahusikajeeee
    pumbaaaaaf zenyuuuuu

    ReplyDelete
  5. hv yanga mbona usajili wenu una shida hv kama hamna hela sii mtulie?

    ReplyDelete
  6. Yanga anaharibu mambo kichaka cha lawama simba, inashangaza sana

    ReplyDelete
  7. Kifaru hata muda wa mkataba wenyewe hajui eti atawasiliana na mtu wa sheria 😂😂 wenye kuendesha timu wameshachukua chao kama haujashirikishwa itakua bahati mbaya

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic