October 11, 2020

 


KIKOSI cha timu ya Azam Media jana Oktoba 10 kilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Karume, Ilala, Dar.

Mchezo huo ambao ulikuwa maalumu kwa ajili ya kuwahamasisha mashabik kujitokeza kwa wingi leo Oktoba 11, Uwanja wa Mkapa ulihudhuriwa na mashabiki wengi waliojitokeza kuona burudani ndani ya uwanja.

Kipindi cha kwanza timu zote mbili zilikwenda mapumziko huku Azam Media ikiwa mbele kwa mabao 2-1 jambo lililowavuruga wachezaji wa Global FC waliokuwa wamejipanga kupata matokeo chanya

Kipindi cha pili kilikuwa na ushindani mkubwa na Azam Media iliweza kufunga mabao mawili mengine  na kuwafanya wawe mbele kwa mabao manne.

Mpaka dakika 90 zinakamilika Uwanja wa Karume, Azam Media ilikuwa inaongoza kwa mabao 4-1 huku Global FC ikiwa na bao moja pekee ambalo lilikuwa la kufutia machozi.

Ushindi huo unawafanya Global FC kurejea chimbo upya kuanza kujiandaa kwa mchezo wa marudio dhidi ya timu ya Azam Media ambao unatarajiwa kuchezwa hivi karibuni.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic