October 13, 2020


 OFISA Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa mashabiki wajitokeze kwa wingi leo Uwanja wa Azam Complex kushuhudia burudani na gongagonga zitakazotolewa kutoka kwa wachezaji wao.


Leo Simba itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Ndanda FC utakaochezwa saa 11:00 jioni ambapo kiingilio kwa mzunguko ni shilingi 7,000, (buku saba). 


Manara amesema:"Wakazi wa jiji la Dar es Salaam hususani kuanzia  wale wa makazi ya Chamazi, Kigamboni, Mbagala wanapaswa watambue kwamba mabingwa wa nchi Simba watashuka uwanjani kucheza dhidi ya Ndanda FC.

"Mechi hii ukiikosa utajitakia magonjwa kwani tutapiga mpira wa visukarisukari na ni uwanja mzuri tunakwenda kucheza sasa sijui unahitaji nini sasa hapo.

"Najua mnatambua kwamba kuna wachezaji wengi wazuri ndani ya Simba hivyo hakuna ambaye hajui namna timu yetu inavyofanya muda wote uwanjani," amesema.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic