Leo Desemba 22, Biashara United imebaki na pointi zote tatu Uwanja wa Karume kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons.
Mabao hayo yote mawili yalifungwa kipindi cha pili baada ya muda wa mapumziko kukamilika kwa timu zote kwenda vyumba vya kubadilishia nguo zikiwa hazijafungana.
Watupiaji wa mabao walikuwa ni Deo Mafie dk 55 na Kelvin Friday dk ya 90 ambaye alikomelea msumari wa mwisho na timu yake kusepa jumla na pointi tatu mazima.
Baraza amesema:"Niliwaambia wachezaji wangu kwamba wana uwezo wa kupata ushindi kwenye mchezo huo ikiwa watatumia makosa ya wapinzani hivyo wanapaswa wawe makini muda wote.
"Nimefurahi kuona kwamba wameweza kutumia makosa ya wapinzani kupata pointi tatu kwetu ni furaha na tunaamini kwamba ni mwendo mzuri ambao tupo nao kwa sasa," .
Huu ndio udhaifu wa hizi timu akina prisons zinakaza na kukamia simba na yanga basi wamemaliza ligi.
ReplyDeleteTrue
ReplyDelete