December 16, 2020


IMEBAINIKA kuwa kiungo mshambuliaji hatari wa Klabu ya Simba, Luis Miquissone amegoma kuondoka ndani ya timu hiyo licha ya matajiri wa Kiarabu kutoka nchini Misri, Klabu ya Pyramids kuonyesha nia ya kuhitaji huduma yake.

Pyramid inaripotiwa kuwa tayari kuvunja mkataba wa Luis na Simba kwa kuweka mezani dau linalokadiriwa kufikia shilingi Bilioni 1.5 za Kitanzania.

Akizungumzia ofa hiyo mmoja wa viongozi wa juu wa klabu hiyo aliyeomba hifadhi ya jina lake amesema Luis alikaa kikao na Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohammed Dewji 'MO' ili kujadili dili hilo, lakini akamjibu bosi huyo kuwa ana furaha kuendelea kuitumikia Simba na wala hana mpango wa kuondoka ndani ya timu hiyo kwa sasa.

"Suala la Luis kuhitajika na Pyramid ni kweli lipo na tayari walishaleta ofa ambayo ilijadiliwa kwa kirefu na Mwenyekiti wa Bodi ambapo, Luis alipewa taarifa ya uwepo wa dili hilo.

"Lakini Luis mwenyewe alimwambia MO kwamba bado ana furaha kuendelea kuichezea Simba kwa misimu mingi zaidi na kwa sasa hana mpango wa kuondoka Simba,".

12 COMMENTS:

  1. Huyo ndie muungwana anaejuwa fadhila na akaona utu na uaminifu ni bora kuliko pesa

    ReplyDelete
  2. Anaipenda simba na ni muungwana sana

    ReplyDelete
  3. Muache asubiri wamchoke,atakuja likumbuka hilo dili,hawajui Simba na Yanga huyo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kweli atajuta sana, hizi timu zetu ni kama Bublish tu, ukiish autamu watu wanatema mbali huko.

      Delete
  4. Figisu ti hakuna cha kukataa wala nn na nyie mmegeuka utopolo kuwafungia milango wachezaji bumbavu

    ReplyDelete
  5. Biashara nzuri sana hii kwenye soka basi tu wabongo hatujitambui

    ReplyDelete
  6. Kuna kuondoka anafka pyramid yanamkuta ya kichuya
    Bora akae tu huenda thaman yke ikapanda zaid

    ReplyDelete
  7. Simba hawa wakatae daunla B1.5 thubutu huyo konde hakifikisha hata 200m acheni kuandika porojo na upuuzi

    ReplyDelete
  8. Hakuna hapa Tanzania club itakayokataa kumuuza mchezaji kwa ofa ya bilioni 1 na nusu, Hawa jamaa wanapika Sana Habar

    ReplyDelete
  9. Simba kama wataacha b1.5 basi watakua hawajui maana halisi ya biashara ktk mpira

    ReplyDelete
  10. Mi simba damu kama kweli IPO iyo of a ya b1.5ni kuchukua tu binge LA biashara hyo

    ReplyDelete
  11. Thamani ya miqson ni kubwa mno bilioni1.5 ni hela kdogo sana,,,kwanza simba wenyewe wamelipa mil700 kuvunja mkataba mamelod sundown bado hela yake ya usjaili kamq zaid ya mil300 alizochukua yy kama mchezaji ,,,,iyo itakua biashara bubu simba wametumia zaidi ya bilion moja kumsajili aje amuuze kwa bil1.5??hamnaga biashara ya kiboya kama iyo,,,simba akifanikiwa kuingia makundi na miqson akikiwaya sana simba watakuja kumuuza kwa zaidi ya bilion4 za kitanzania

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic